ABDU ROGO.TAFSIRI YA SURAT-TAUBA. 5

ABDU ROGO.TAFSIRI YA SURAT-TAUBA. 3

ABDU ROGO.TAFSIRI YA SURAT-TAUBA. 2

TAKWIMU YA QURAN

            TAKWIMU YA QUR-AANI TUKUFU.

Qurani tukufu ni kitabu cha pekee cha mwenyezi mungu alicho mteremshia mtume Muhammad s.a.w ambacho kimebaki na kitaendelea kubaki bila kuongezwa au kupunguzwa sura, aya, neno, au hata herufi yake moja. Kwa mujibu wa idadi iliyo tolewa na sheikh Bahai katika kitabu chake kiitwacho al-kashkuw, qurani ni kitabu chenye jumla ya sura 114, aya6236, maneno 76,440 na herufi 322,373.

Idadi ya kila herufi katika Qurani ni hii;
1. ALIF     40,792
2.BAA       1,140
3.TAA       1,299
4.THAA    1,291
5.JIIM       3,293
6.HAA    9,997
7.KHAA    2,419
8.DAAL      10,903
9.DHAAL    4,840
10.RAA        10,903
11.ZAA           9,583
12.SIIN        4,091
13.SHIIN     20,133
14.SAAD      1,274
15.DHAAD    1,200
16.TWAA      840
17.DHWAA     9,220
18.A,AYNI      7,499
19.A,GHAYNI    1,120
20.FAA            8,497
21.QAAF        5,240
22.KAAF        2,500
23.LAAM      26,019
24.MIIM     20,560
25.NUUN        20,360
26.WAAW        13,700
27.HEE(HAA)    700
28.YAA(YEE)     502

          WALLAHU AALAM*******YURY'S LAW

HIJJA

                           ELIMU YA HIJJA

Hijja ni nini?
Hijja ni kuikusudia nyumba ya mwenyezi mungu (ilioko makka) kwa ajili ya mambo ya hijja (Nusuki)

Ni mambo yepi hayo (Nusuki)?
Mambo hayo ni vitendo vyote vya hijja kama vile nguzo zake na wajibu wake.

Nguzo zake ni ngapi?
Nguzo za hijja ni tano, ambazo ni;
1.ni kuhirimia pamoja na kutia nia 
2.kusimama Arafa
3.kutufu( kuizunguka ) Al-ka'ba mara saba
4.kwenda baina safa na mar-wa mara saba
5.kunyoa au kupunguza nywele za kichwani.

Wajibu wa hijja ni mambo mangapi?
wajibu wa hijja ni mambo matano, ambayo ni ;
1.Kuhirimia katika kituo
2.kurembea magino matatu
3.kupitiwa na usiku ( kulala) muzdalifa.
4.kupitwa na usiku (kulala) mina siku za mwezi 11, 12 na 13 za mfungo tatu
5.Tawafu ( kuizunguka Al-ka'ba ) kwa kuaga kwa anae ondoka makka

Ni mambo mangapi hua haramu baada ya kuhirimia?
mambo kumi hua ni haramu kwa mtu alie hirimia,
1.kuvaa nguo ilio shonwa
2.kufunika kichwa kwa mwanamme na kufunika uso kwa mwana
3.kuchana nywele au kuzitia mafuta
4.kunyoa nywele
5.kukata kucha
6.kujipamba au kujitia manukato
7.kumuua mnyama kwa kumuwinda
8.ndoa
9.kufanya tendo la ndoa
10.kukumbatiana kwa matamanio

        WALLAHU AALAMU*******YURY'S LAW.

FUNGA.

                    ELIMU YA FUNGA.

Funga ni nini?
Ni kujizuilia na kula na kunywa, kuingilia/ au kuingiliwa (kufanya tendo la ndoa) na kila jamboleny kufuturisha kuanzia inapo chomoza alfajiri mpaka linapo zama jua, kwa siku zote za mwezi wa Ramadhani.

Ni nani anawajibika kufunga?
Ni wajibu kwa kila muislamu aliye baleghe, mwenye akili timamu, anaye weza (huko kufunga ) na alie toharika kutokana na hedhi na nifasi.

Faradhi za funga ni ngapi?
Faradhi za funga ni mbili;
1. nia
2.ni kujizuilia na yenye kufuturisha  ( yenye kufunguza)

Ni yepi hayo yenye kufuturisha?
Ni kila jambo lenye kubatilisha funga, nayo ni mambo manane;
1.kuingiza kitu ndani kwa makusudi (katika tundu za mwili)
2.kujitapisha kwa makusudi
3.kupatwa na hedhi
4.nifasi
5.kujitoa manii kwa makusudi
6.kufanya tendo la ndoa
7.kuritadi (kutoka katika uislaamu)
8.kuwa na wazimu

Ni siku zipi haramu kufunga?
siku hizo ni
1.siku za Idd mbili ( Idil-fitri na Idil-hajj)
2.siku za mwezi 11, 12 na 13 katika mfungo tatu 
3.siku ya shaka, isipokuwa itapo wafikiana na ada yake ( ya kufunga katika siku hiyo) au kuunganisha na funga ilio kabla yake.

           WALLAHU AALAMU*******YURY'S LAW.

ZAKATUL-FITRI

                                 ZAKATUL-FITRI

Zakatul-fitri ni nini?
Ni vibaba vinne vya chakula (kinacho pendwa sana) katika mji.

Ni nani anae wajibika kutoa Zakatul-fitri?
Anae wajibika kutoa zakatul-fitri ni kila muislamu alie huru ambae ana ziada katika chakula chake( cha siku ya Idd) kwa ajili yake yeye na walio mlazimu yeye kuwalisha miongoni mwa waislamu. Na atatoa kwa ajili yake, na pia awatolea wale waislamu . yeye kuwalisha miongoni mwa waislamu.

Ni wakati gani ni wajibu kutoa zakatul-fitri?
Zakatul-fitri hutolewa kuanzia magharibi ya siku ya mwisho wa Ramadhani.

   WALLAHU AALAMU*******YURY'S LAW.

ZAKA.

                                            SOMO LA ZAKA.
Nini maana ya zaka?
Zaka ni kutoa kiwango maalumu cha mali mahsusi na kuwapa wanaopasa (kuwapa hiyo zaka) katika mbea nane au mbea moja miongoni mwa hizo.

Ninani hao mbea nane wanaopasa(kupewa zaka)
Hao ni wale walio tajwa katika qurani, kwa kauli yake mwenyezi mungu katika surat Tauba aya ya 60, amesema Allah" sadaka hupewa (watu hawa) ; mafakiri na masikini na wanaozitumikia na wanao tiwa nguvu nyoyo zao (juu ya uislamu) na katika kuwapa uungwana watumwa na katika kuwasaidia wenye deni na kwa ajili ya mwenezi mungu na msafiri alie haribikiwa "

Ni wepi hao mafakiri?
Hao ni wale ambao hawana mali wala chumo linalo watosheleza kwa haja zao za lazima.

Ni wepi hao masikini?
Hao ni wale wenye mali au chumo lakini hawajitoshelezi kwa haja zao za lazima.

Ni wepi hao wanao ifanyia kazi zaka?
Hao ni wale wanao kusanya zaka na kuigawa kwa wanao pasa (kupewa zaka)

Ni wapi hao wanao tiwa nguvu nyoyo zao (juu ya uislamu)?
ni wale walio silimu karibu.

Ni wepi hao wenye kupewa uungwana?
Ni wale watumwa walio andikwa( kuachwa huru ).

Ni nani hao wenye madeni?
Hao ni wale wenye madeni ambayo hawawezi kuyalipa.

Ni wepi hao walio katika njia ya mwenyezi mungu?
Ni wale wanao jitolea katika njia ya mwenyezi mungu ( kwa ajili ya kutaka radhi za mwenyezi mungu)

Ni wepi walio haribikiwa njiani?
Hao ni wasafiri ambao hawasafiri kwa ajili ya maasi na hawana mali inayo watosheleza katika safari yao.

Ni kitu gani kilicho wajibu kukitolea zaka?
ni wajibu kwa: 1.wanyama wanao fugwa(ambao ni halali)
                        2.dhahabu na fedha
                       3.vipando
                      4.matunda
                     5.mali ya biashara

Ni wepi wanyama hao?
Hao ni ng'ombe, mbuzi, na kondoo, nyati na ngamia .

Nini shuruti za wanyama hao?
shuruti za wanyama hao ni Nisab, Sawm na Hawli

Nisab ni nini?
Ni kipimo maalumu cha kisheria

Sawm ni nini?
Ni kula wanyama hao katika ardhi isiyo milikiwa na mtu yeyote.

Hawli ni nini?
Huko ni kupita mwaka mmoja kamili.

Nini shuruti za zaka ya dhahabu na fedha, na mali ya biashara?
Shuruti zake ni Nisab na Hawli.

Ni matunda gani ambayo hutolewa zaka?
matunda ambayo hutolewa zaka ni Tende na Zabibu

Ni vipando gani ambavyo hutolewa zaka?
Ni kila kinacho liwa kama Mchele na Ngano.

Ni nini shuruti za zaka ya vipando na matunda?
Ni Nisab tu ( kufikia kiwango maalum)

      WALLAHU AALAMU*******YURY'S LAW.

SALA YA JENEZA.

                                SALA YA JENEZA (SALA YA MAITI)

Mambo gani ni wajibu kufanyiwa maiti?
Ni wajibu kufanyiwa matayarisho, nayo ni;
        1.kukoshwa
        2.kukafiniwa
        3.kusaliwa
        4.kuzikwa.

Vipi husaliwa sala ya maiti?
1.Anuilie anaesali  kuwa anamsalia huyo maiti pamoja na kupiga takbir-Allahu akbar
2.ASome suratil faatiha
3.Aseme Allahu Akbar
4.Amsalie mtume S.a.w
5.Aseme Allahu akbar
6.Amwombee dua maiti
7.Aseme Allahu Akbar
8.Atoe salamu

             WALLAHU AALAM*******YURY'S LAW

SALA YA MSAFIRI

                            SALA YA MSAFIRI.

Vipi atasali anae safiri?
Inajuzu kwa msafiri kupunguza rakaa mbili kwa sala Adhuhuri, laasiri na Isha. Na pia inajuzu kuzichanganyisha ( kuzisali kwa pamoja) sala ya Adhuhuri na laasiri, na magharibi kuisali pamoja na Isha kwa wakati mmoja. inajuzu kufanya hivyo kwa kutanguliza au kuchelewesha.

Ni ipi nia ya sala ya msafiri?
nia yake ni ; nina sali sala ya faradhi ya adhuhuri, rakaa mbili kwa kutanguliza pamoja na kukusanya ( au kuchelewesha pamoja na kujumuisha) kwa hali ya kupunguza kwa ajili  ya mwenyezi mungu ( allahu akbar)

                  WALLAHU AALAM*******YURY'S LAW

SALA YA JAMAA

                             SALA YA JAMAA.

Ninini hukumu ya sala ya jamaa?
Ni faradhi kifaya kwa wanaume wakaazi wa mji na uchache wake ni Imamu na maamuma.

Shuruti za sala ya jamaa ni ngapi?
shurti zake ni saba, ambazo ni;
     1.maamuma anuie kumfuata imamu
     2.maamuma ajue vihamo vya imamu japo kwa msaada (kwa kusikia sauti au kuona safu za mbele)
    3.maamuma asiwe mbele ya imamu
   4.Amkaribie Imamu ikiwa si msikitini
    5.kusiwe na kizuizi baina yao
    6.Maamuma amfuate imamu wake
    7.Asimfuate yule ambaye itamlazimu kuja kuilipa( kuirejea) sala (baadae)

                             WALLAHU AALAM*******YURY'S LAW.

SALA.

                                                MAFUNDISHO YA SALA.

Nani inamlazimu sala?
Sala humlazimu kila muislamu alie baleghe, mwenye akili timamu, na ni juu ya waliii wa mtoto(mzee)kumuamrisha kusali baada ya kutimia umri wa miaka saba na kumpiga pindi akiwacha(kusali)baada ya kutimia umri wa miaka kumi.

sharti za sala ni ngapi?
sharti za sala ni tano, ambazo ni;
    1.kujitaharisha(kwa kuepukana)na hadathi kubwa na ndogo .
    2.kutahirika kwa kiwili wili,nguo na pahala pa kusalia(kutokana) na najisi.
    3.kustiri utupu.
     4.kujua kuingia kwa wakati.
     5.kuelekea kibla.

Idadi ya rakaa za witri ni ngapi?
Idadi ya rakaa za witri ni kumi na moja na wakati wake ni baada ya sala ya insha hadi kuchomoza alfajiri.

Nyakati ngapi hua ni haramu kusali?
Hua ni haramu kusali katika nyakati tano, ambazo ni :
      1.wakati wa kuchomoza jua mpaka linyanyuke kiasi cha mkuki.
      2.wakati jua linapokuwa lipo sawa sawa na kitu(saa sita) isipokuwa siku ya ijumaa, mpaka lipinduke jua.
      3.wakati jua linapo kuwa manjano mpaka linapo kuchwa( magharibi).
      4.baada ya sala ya alfajiri mpaka lichomoze jua.
      5.baada ya sala ya alaasiri mpaka lichwe jua.

Nguzo za sala ni ngapi?
Nguzo za sala ni kumi na nne.ambazo ni
   1.kusimama kwa anae weza katika sala ya faradhi.
   2.nia
   3.takbiratul ihram
   4.kusoma suratil faatiha
   5.kurukuu
   6.kujituliza( katika rukuu, itidali na sijda)
   7.itidali
   8.kusujudu
   9.kukaa kitako baina ya sijda mbili
  10.kukaa kitako kwa ajili ya tahiyatu ya mwisho
  11.tahiyatu ya mwisho
  12.kumsalia mtume katika tahiyyatu ya mwisho
  13.salamu ya kwanza
  14.utaratibu ( kwa mpangilio wake huu kuanzia nguzo ya 1-13)

**itidali ni kisimamo baada ya kutoka katika rukuu kabla ya kusujudu.

Ni zipi sunna za sala kabla yake
Sunna za kabla au nje ya sala ni Adhana na Iqama.

Ni zipi sunna za ndani ya sala?
Sunna za ndani ya sala zipo aina mbili ambao ni ; Ab'adh na hay-ati

Sunna za Ab'adh za sala ni ngapi?
Sunna hizo ni tatu, ambazo ni ;
     1.Tahiyyatu ya kwanza
     2.kumsalia mtume katika tahiyyatu ya kwanza
     3.kunuti katika sala ya asubuhi na katika sala ya witri kwenye nusu ya pili ya mwezi wa ramadhani
   
Sunna za hay-ati ni ngapi?
Sunna za hay-ati ni kumi na tano , ambazo ni ;
    1.kunyanyua mikono miwili sawa na mabega wakati wa takbiratul ihram, wakati wa kurukuu, wakati wa itidali, na wakati wa kusimama kutoka katika tahiyyatu ya kwanza.
    2.kuweka mkono wa kulia juu ya mkono wa kushoto chini ya kifua au juu ya kitovu.
    3.Dua ya kufungulia sala
    4.kusoma " Audhu billahi minashaytani......
    5. kuitika Amin
    6.kusoma sura baada ya suratil faatiha katika rakaa ya kwanza na ya pili
    7.kudhihirisha sauti katika mwahala mwake na kutodhihirisha sauti  mwahala mwake.
    8.kusema Allahu akbar wakati wa kuinama ( kwenda katika rukuu) na wakati  wa kunyanyuka.
    9.kusema samiallahu liman hamidah katika itidali
   10.kusema sub-haana rabbial Adhiym katika rukuu mara tatu, na kusema sub-haana rabiyal A'la katika sijda mara tatu.
    11.kuweka mikono miwili juu ya mapaja hali ya kuukunjua mkono wa kushoto na kuukunja wa kulia isipokuwa kidole cha shahada.
     12.kuukalia mguu wa kushoto ( katika vitako vilivyomo katika sala)
     13.kuupitisha mguu wa kushoto utokezee kuliani ( na kulikalia tako la kushoto ) katika tahiyyatu ya mwisho.
     14.salamu ya pili
     15.Nia ya kutoka katika sala

Ni yepi mambo yenye kubatilisha sala?
Mambo yenye kubatilisha sala ni manne,ambayo ni ;
    1.kusema kwa kukusudia
    2.kufanya vitendo vitatu mfululizo
    3.kula au kunywa
   4.kuacha nguzo miongoni mwa nguzo za sala au kukosa shuruti miongoni mwa shuruti za sala.

Ninini hukumu ya alie acha nguzo ya sala kwa kusahau?
Ataileta nguzo hiyo atakapo ikumbuka na atasujudu " sijdatis-sahwi"

Ninini hukumu ya alie acha sunna kwa kusahau?
hatailipa sunna hiyo bali atasujudu sijidatus-sahwi

Ninini hukumu ya alie acha sunna ya hay-ati?
Hataileta hiyo sunna wala hataleta sijidatus-sahwi.

Ninini hukumu ya asie weza kusimama katika sala ya faradhi?
Atasali kwa kukaa kitako, akishindwa atasali kiubavu ubavu, akishindwa atasali kichali chali, ama sala ya sunna inajuzu kwa mwenye kuweza kuisali kwa kukaa, au kusimama au kiubavu ubavu.

             wallahu allamu*******yury's law

KUTAYAMMAMU.

                                                     KUTAYAMMAM.

Nini maana ya kutayammam?
Kutayammamu ni kupangusa uso na mikono kwa mchanga ulio safi (tohara) badala ya kutawadha au kuoga ( kwa kutumia maji).

Faradhi za kutayammam ni ngapi?
Faradhi za kutayammam ni tano,
       1.nia
       2.kuhamisha mchanga kuufikisha kwenye kiungo chenye kupanguswa
       3.kupangusa uso
       4.kupangusa mikono miwili mpaka kwenye vifundo viwili
        5.kufuatanisha 

Ni wakati gani inapaswa kutayammamu?
Inapasa kutayammamu iwapo:
    1.yanapo kosekana maji
    2.inapo hofiwa kutumiwa maji kwa baridi au ugonjwa
   3.yanapo hitajika kwa ajili ya kiu ( kunywa) wanyama watukufu

Ni mambo gani hubatilisha kutayammam?
Hubatilika kutayammam kwa yale yote yenye kubatilisha udhu na kuyaona  maji unapo ingia wakati wa sala na kuritadi.
                                        wallahu aalamu.
  yury's law.

KUOGA

                                            KUOGA
Kuoga ni nini?
Kuoga ni kuosha kiwili wili chote kuanzia juu ya kichwa hadi mwisho wa nyayo zake.

Faradhi za kuoga ni ngapi?
Faradhi za kuoga ni tatu, ambazo ni;
            1.kutia nia wakati wa kuosha sehemu ya mwanzo ya kiwili wili
            2.kuondosha najisi kwenye kiwili wili
            3.kufikisha maji katika sehemu yote ya mwili pamoja na nywele.
   
Ni ipi nia ya kuoga?
Ni kusema: nanuia kuoga kwa ajili ya kuondosha hadathi kubwa,lakini nia hiyo haitakiwi itamkwe kwa ulimi ila inatakiwa iwe ndani ya moyo wako.

Ni ipi hadathi kubwa?
Hadathi kubwa ni kila yenye kuwajibisha kuoga.

Ni yepi yenye kuwajibisha kuoga?
Yenye kuwajibisha kuoga ni JANABA, HEDHI, NIFASI, KUZAA, NA KUFA.

Je, janaba ni nini?
janaba ni josho linalo patikana baada ya kugusana tupu mbili au kutokwa na manii kwa kusudia au bila kukusudia .

Nini hedhi?
Hedhi ni damu yenye kumtoka mwanamke baada ya kutimia miaka 9 kwa ajili ya uzima na ada ya kila mwezi.

nifasi ni nini?
Nifasi ni damu inayo mtoka mwanamke baada ya kuzaa.

mambo gani ni haramu kwa mwenye janaba?
Niharamu kwa mwenye janaba: kusali, kutufu, kugusa msahafu, kusoma qurani na kukaa muskitini.

Ni mambo gani ni haramu kwa mwenye hedhi na nifasi?
Ni haramu kwa mwenye hedhi na nifasi kusali, kufunga na kufanya yale yote yalio haramu kwa mwenye janaba.

                                        wallahu aalamu.
yury's law.

UDHU.

                                                              FARADHI ZA UDHU.
Faradhi za udhu ni ngapi?
katika uislamu faradhi za udhu ni sita, ambazo ni:
           1.kutia nia wakati wa kutawadha
            2.kuosha uso
            3.kuosha mikono miwili mpaka kwenye vifundo viwili
            4.kupaka maji sehemu ya kichwa au nywele za kichwa mpaka uguse ngozi
            5.kuosha miguu miwili mpaka kwenye vifundo viwili
            6.kufuatanisha( utawadhe kwa kufuata utaratibu ulio pangwa kuanzia 1-6)

Sunna za udhu ni ngapi?
sunna za udhu ni nyingi, kati ya hizo ni:
       1.kupiga Bismillahi
       2.kupiga mswaki
       3.kusukutua
       4.kupandisha maji puani
       5.kupangusa(kupaka) maji kichwa kizima
       6.kupangusa masikio mawili nje na ndani
       7.kuzichambua ndevu kama ni nyingi
       8.kuasua( kuvichanua) vidole viwili vya mikono miwili na miguu miwili
       9.kutanguliza kulia kabla ya kushoto
       10.kufanya mara tatu tatu
       11.kufuatanisha
       12.kuomba dua baada ya kutia udhu.

Mambo mangapi hutengua udhu?
Udhu hutenguka kwa mambo matano, ambayo ni:
            1.kutokwa na kitu kwenye moja kati ya njia mbili( TUPU MBILI)
            2.kulala bila kuambatanisha makalio yake kwenye ardhi
            3.kutokwa na akili kwa kulewa au wazimu au kuzimia
            4.kumgusa mwanamke unae weza kumuoa pasi na kizuizi
           5.kugusa utupu kwa matumbo ya viganja
           
Niyepi makuruhu ya udhu?
makuruhu ya udhu ni kutumia maji ovyo, kuzungumza mazungumzo yasio na maana au kutaka msaada kwa mtu mwingine.

Ni mambo gani ni haramu kwa mwenye hadathi ndogo?
mambo ambayo ni haramu kwa mwenye hadathi ndogo ni :
      1.kusali
      2.kutufu
       3.kugusa msahafu

                                                     WALLAHU AALAM.
YURY'S LAW.

KUSTANJI

                           KUSTANJI KATIKA UISLAAMU.
Kustanji ni nini?
kustanji ni kukosha njia mbili ( tupu mbili) kwa maji kwa kuondosha chenye kutoka humo kama mkojo na mavi.

Je, inajuzu kustanji kwa jiwe?
inajuzu kustanji kwa mawe matatu mpaka iondoke najisi pale ilipotoka .
                                                           
                                                        yurys law.
                                                WALLAHU AALAM

NAJISI

Najisi ni zipi?
Najisi ni damu, usaha, matapishi, ulevi, mbwa, nguruwe, na maziwa ya mnyama isiyo liwa nyama yake na chenye kutoka kwenye njia mbili( tupu mbili ) isipo kuwa manii kwani hayo ni ( tohara ) na maiti, manyoya yake na mifupa yake ( vyote ni najisi ) isipokuwa maiti ya binaadamu, samaki na nzige.

vipi hutoharika najisi?
nijisi hutoharishwa kwa kukoshwa mahala ilipo ingia najisi kwa maji yalio tohara mpaka iondoke harufu yake na rangi yake na ladha yake ( isipo kuwa najisi ya mbwa na nguruwe na ngozi ya maiti)

Vipi hutahirika najisi ya mbwa na nguruwe?
Najisi ya mbwa na nguruwe hutahirika kwa kukoshwa mahala ilipo kuwa najisi mara saba, moja kati ya hizo kwa mchanga.

Vipi hutoharika ngozi ya maiti?
Ngozi ya maiti hutoharika kwa kudubaghiwa ( kukaushwa ).
                                                yurys law. 
                                         WALLAHU AALAM.


TOHARA

Tohara ni nini?
tohara ni kitendo ambacho haitosihi sala pasi na kukifanya kama kuondosha najisi, kustanji, kutawadha, kukoga(josho), kutayammam.

Njia za tohara ni zipi?
Njia za tohara ni maji, mchanga, jiwe, kudubaghi( kukausha) kama ngozi na (sabuni)

Niyepi maji ambayo yanafaa kujitoharishia?
Ni kila maji ambayo huteremka kutoka mawinguni au yanayotoka(bubujika) ardhini yasiyo najisi wala yaliotumiwa.

Niyepi maji yaliyo najisika?
Ni maji yaliyo kidogo ambayo yameingia najisi ndani yake.

Ni yepi maji yalio tumika?
Ni maji kidogo yalio tumiwa katika kuondosha hadathi au najisi.

Ni yepi maji kidogo?
Ni maji yasiyo timia kulla mbili

Ni yepi maji mengi?
Ni maji yaliyo timia kulla mbili na zaidi.

Ni nini kulla mbili?
Kulla mbili ni maji yaliyo kiasi cha wakia 148 au yaliyo katika sehemu ambayo huenea birika la maji lenye pembe nne lenye urefu wa dhiraa moja na robo kwa marefu ya kwenda juu na mapana ya kwenda chini ( urefu wa kwenda chini).
                                             wallahu aalamu.

HUKUMU ZA UISLAMU.

Hukumu za uislamu ni ngapi?
Hukumu za uislamu ni tano, ambazo ni FARADHI, SUNNA, MUBAHA, HARAMU NA MAKRUHU

Faradhi ni nini?
Faradhi ni lile lililolazima kulifanya na atakapo lifanya mukallaf hupata thawabu na atakapo liwacha hupata dhambi (adhabu ).

Aina za faradhi ni ngapi?
faradhi zimegawanyika katika aina kuu mbili, ambazo ni faradhi ya lazima na faradhi ya kutosheleza.

Ni ipi faradhi ya lazima?
Faradhi ya lazima ni ile ilio lazima juu ya kila mukallaf kuifanya, kama vile kusali na kufunga.
mukallaf ni mtu alie baleghe mwenye akili timamu.

Ni ipi faradhi ya kutosheleza?
Faradhi ya kutosheleza ni ile iliyo lazima kwa mukallafina wote kuifanya lakini itakapo fanywa na mukallaf baadhi kati yao basi wote hupata thawabu.
faradhi hii sio lazima ifanywe na kila mtu ila watapo ifanya wachache basi huesabika kuwa watu wote wameitekeleza faradhi hiyo.

Sunna ni nini?
ni jambo linalo pendezeshwa kulifanya ,na mwenye kulifanya hupata thawabu na mwenye kuliwacha hapati dhambi.

Mubaha ni nini?
mubaha ni lile ambalo inajuzu kwa mtu kulifanya na kuliwacha, na mwenye kulifanya hapati thawabu na pia mwenye kuliwacha hapati dhambi.

Haramu ni nini?
Haramu ni jambo lililolazima kwa kila mukallaf kuliwacha, na mwenye kuliwacha hupata thawabu lakini pia mwenye kulifanya hupata dhambi. kama vile kunywa ulevi n.k

Makruhu ni nini?
Makruhu ni jambo linalo pendeza kuliwacha na mwenye kuliwacha hupata thawabu, lakini pia mwenye kulifanya hapati dhambi.
                                      wallahu aalam.

KUHUSU GHADHABU

  Hakika ghadhabu hutokana (asili ya ) ya shetani, na hakika shetani kaumbwa kutokana na moto, na hakika moto unazimwa kwa maji, basi akighadhibika mmoja wenu na akatawadhe au anywe maji na ikiwezekana anyamanze kisha amlani shetani na kama hawezi kukaa katika sehemu hiyo basi aondoke penye mzozo huo ulio msababishia hiyo ghadhabu.

Mtume s.a.w atakae zuwia ghadhabu na yeye anaweza kuizuia basi ataitwa na mwenyezi mungu mtukufu juu ya vichwa vya viumbe siku ya kiama ( ewe fulani ), achagua katika mahurul-aini ( wanawake wa peponi ) ampendae.

Kwahiyo ndugu zangu tujifunze kuzuia hasira zetu ili tueze kufanikiwa siku ya qiyama, AAMIN.

FAIDA YA ASALI


Asali inafahamika vema Duniani kote kama mojawapo ya silaha ya kiajabu katika kupigana na magonjwa na matatizo yatokanayo na uzee. Sasa hivi, utafiti mpya umeonyesha kwamba uwezo wa asali unaweza kuongezwa maradufu kama itachanganywa na mdalasini wa kawaida.

Uchunguzi wa kina ufanywao kwa wiki na jarida la World News wa Tiba, wataalamu wa madawa yatokanayo na mimea pamoja na kijarida cha afya na lishe, imeonekana kwamba kuna dazani nyingi za umuhimu wa asali na mdalasini pamoja na michanganyiko {dawa} ya kusisimua iletayo afya bora.


Kama ifuatayo:
1. Ugonjwa wa Viungo/Maumivu na Uvimbe {ARTHRITIS}.
Wataalamu wa lishe wanapendekeza kuchukua kwa kutumia mchanganyiko wa sehemu moja ya asali pamoja na sehemu mbli za maji vuguvugu na kijiko kimoja {cha chai} chenye mdalasini - na kuchua sehemu zilizoathirika. Nafuu hupatikana katika muda wa dakika moja.


Vinginevyo tengeneza chai-kikombe kimoja chenye maji moto, weka vijiko vya chakula -viwili vya asali kwa kijiko cha chai cha mdalasini. Kunywa asubuhi na jioni ili kuondoa maumivu.


Katika tafiti iliyofanyika hivi karibuni na chuo kikuu kimoja huko Copenhagen, madaktari waliwapa wagonjwa 200, {syrup} mchanganyiko wa kijiko kimoja *cha chai* cha asali na kimoja cha mdalasini kila asubuhi kabla ya kifungua kinywa. Asilimia 73% yao waliripoti nafuu kubwa ya maumivu yao na ongezeko katika kufanya shughuli kama kujongea na kutembea vyema.


2. kukatika kwa nywele {HAIR LOSS}
Asali ikishachanganywa na mdalasini pamoja na mafuta vuguvugu ya olive, hutoa kichocheo maridhawa cha kuotesha nywele kinachotumika katika dawa ya Dork. Mchanganyiko huo vuguvugu unapakwa kwa kusugua kichwani na kuachwa kwa dakika 15.



3. Ukungu wa miguuni {FUNGUS}
Changanya kijiko kikubwa cha mezani cha asali, vijiko viwili vya mdalasini {vya chai}. Pakaa sehemu zilizoathirika usiku kwa muda wa nusu saa, kisha safisha kwa sabuni na maji. Shida yako itakwisha kwenye kipindi cha wiki moja.



4. Maambukizo kwenye kihofu cha mkojo {BLADDER INFECTION}
Bilauri ya maji vuguvugu yaliyochanganywa na vijiko viwili {vya chai} vya mdalasini na kijiko kimoja {cha chai} cha asali huondoa bacteria kwenye kibofu. Unaweza ukatumia juisi ya cranberry badala ya maji ikiwa ambukizo la kibofu linakuwa sugu.



5. Maumivu ya jino {TOOTHACHE}.
Changanya sehemu tano za asali, na sehemu moja ya mdalasini na tumia kwa maumivu ya jino.
Dondoshea kwenye jino au meno yaliyoathirika hadi maumivu yatakapotoweka.



6. Vidonda vitokanavyo kwa mgonjwa kulala kwa muda mrefu {CANKER
SORES}.
Saladi ya kupaka vidonda iliyochanganywa na asali pamoja na mdalasini kwenye chai ya raspberry
nyekundu ni dawa nzuri ya kuondoa maumivu makali ya canker sores.


7. Helemu {CHOLESTERAL}
Kipimo cha helemu cha watu waliokuwa na afya nzuri {katika jaribio} kilishuka kwa wastani wa asilimia 10 katika muda pungufu ya masaa mawili baada ya kunywa bilauri moja {ounce 16} yenye vijiko viwili vikubwa vya mdalasini iliyochanganywa na chai ya moto. Kinywaji hiki kutwa mara tatu kilifanya kazi nzuri ya kushusha kiwango cha helemu mwilini.


Madhara yaletwayo na vyakula vyenye mafuta yanaweza kudhbitiwa kwa matumizi ya mara kwa mara ya chai hii pamoja na chakula chako. Hii imeripotiwa na mtafiti maarufu Dr Alexander Andreyed na Eric Vogelmann.


Ugunduzi wao uliyakinishwa kwenye jarida mashuhuri la kitiba la Denmark July 1994. vilevile/ aidha uchunguzi mwingine ulibayanishwa kutoa matumizi ya kila siku ya asali safi hupunguza viwango vya helemu.


8. Mafua {COLDS}

Mafua yameshaeleweka ya kwamba hupotea/huondoka baada ya masaa machache baada ya waathirika kutumia kijiko kimoja {cha mezani} cha asali vuguvugu iliyochanganywa na robo kijiko{cha chai} cha mdalasini, mchanganyiko huu ni mahususi katika kusaidia kuondoa chafya na kuvimba koo. 



9. Ugumba {INFERTILITY}
Asali inaaminika kuamsha nyege na wapenzi wa jinsia zote mbili wanashauriwa kunywa anglao vijiko viwili {vya mezani} kila siku kabla ya muda wa kulala {usiku}


Mdalasini umetumika kwa muda mrefu kwenye dawa za kihindi na kichina ili kuongeza uwezo wa uzazi kwa kina mama wenye kuhitaji kuzaa.


Kiungo hiki {mdalasini} huchanganywa na kiasi cha asali na kufanya mgando {paste} ambao hupakwa kwenye fizi za meno na kunyonywa na kuingia mwilini taratibu.


Familia moja iliyokuwa haina watoto iltumia mgando huu kwa mafanikio na kupata mapacha wa kike baada ya kushindwa kwa muda wa miaka 14 kupata mtoto. Walikuwa wameshakata tamaa ya kupata mtoto hadi waliposikia kuhusu mchanganyiko huu wa asali na mdalasini.


10.Mchafuko wa tumbo {UPSET STOMACH}

Asali imetambuliwa kwa kipindi kirefu kama dawa ifaayo kuondoa mchafuko wa tumbo pamoja na kichefuchefu. Ongeza kiasi kidogo cha mdalasini na hii tiba ya kimaajabu vilevile itapunguza maumivu yaletwayo na vidonda vya tumbo.ll.Esidi/Gesi-Co2. Hco3. Hcl.

Kula asali pamoja na mdalasini huweza kuondoa mchafuko wa tumbo na utumbo uletwao na gesi kwa mujibu wa uchunguzi mahsusi iliofanywa huko India na Japan.

12.Ugonjwa wa Moyo {HEART DISEASE}

Unaweza kukinga kupata ugonjwa wa moyo na kuzuia mkusanyiko wa mtandao wa mafuta kwenye mishipa ya damu kwa kula asali na mdalasini mara kwa mara-kwa kupakaa wakati wa kifiingua kinywa.

Kula asali ya mkate wa ngano yenye nyuzinyuzi nyingi iliyopakwa kijiko kimoja {cha mezani} cha
mchanganyiko huo hapo juu kila siku. Tiba hii ya maajabu iliweza kupunguza kuganda kwa mishipa ya damu kwa 74% ya wagonjwa waliokuwa katika nyumba za kutunzia wagonjwa - utafiti mmoja ulionyesha.

13. Shinikizo la damu {HIGH BLOOD PRESSURE}

Shinikizo la damu pamoja na matatizo yaambatanayo ya maumivu ya kifua na kizunguzungu yalitoweka kutoka kwa wagonjwa wengi wiki chache tu baada ya watafiti wa kitaliano kuwapa dozi za mara kwa mara za asali ilyochanganywa na mdalasini. Vipimo vya shinikizo la damu vilionyesha


ukawaida na wote 137 waliofanyiwa jaribio hilo waliripoti kujisikia vyema/vizuri baada ya wiki chache za tiba hii ya ajabu.

14.Kinga ya mwili {IMMUNE SYSTEM}
Kinga yako ya mwili itaongezeka mara tatu zaidi ikiwa utatumia mara kwa mara asali na mdalasini kwa pamoja - wataalamu wanasema.



Utafiti wa kitiba unaonyesha kwamba hazina kubwa ya vitamini{vivurutubisho} na madini pamoja na michanganyiko mingine iondoayo magonjwa pamoja na kinga itolewayo na chembechembe nyeupe za damu, husaidia kuzuia magonjwa pamoja na kuharibu vimelea {virus} na {bacteria}.


15.Ukosefu wa nguvu za kiume [Uhanithi]{IMPOTENCE}
Asali ina historia ndefu ya kuamsha uume pamoja na kuwa dawa madhubuti ya kuponyesha uhanithi.

Kutokana na uwezo wake kama kiamshaji/chaji, asali ilipigwa marufuku kwa makasisi katika baadhi ya dini za kimashariki mwa Dunia. Mwaka jana, watafiti wa kiaustralia waligundua kwamba asali ina uwezo wa kupeleka mwili kutoa homoni mbalimbali kama ilivyo kwa mdalasini, katika Africa na dunia ya kusini, mabaharia wamekuwa wakipaka asali katika sehemu zao za nje ya uume ili kuongeza stamina zao za kufanya mapenzi.


16.Kutokuchaguliwa kwa chakula {INDIGESTION}
Vijiko viwili vya asali iliyonyunyiziwa mdalasini kabla ya mlo{kula chakula} huondoa kiungulia na wataalamu wanasema kwamba asali husaidia kutolewa kwa juisi zinazotumika kuchaguliwa kwa vyakula tumboni na mdalasini unaongeza spidi ya kuchaguliwa kwa vyakula.



17.Flu {INFLTJENZA}
Tafiti moja ya kihispania imethibitisha kwamba aina ya dawa moja asilia ya ajabu ambayo huharibu vairasi {vimelea} waletayo Flu.



18.Umri wa kuishi {LONGERVITY}

Unaweza kuishi kufikia hadi miaka 100 na kufurahia maisha ya afya na madhubuti kwa kunywa kila siku kikombe baridi cha chai ya mdalasini na asali. Kutengeneza kinywaji hiki kitamu, weka vijiko vine{vikubwa} vya mdalasini katika vikombe vitatu vya maji na koroga kwa dakika 10. kunywa robo kikombe kutwa mara tatu au nne na hivyo utakuwa na kinywaji kingi.


19.Chunusi {PIMPLES}

Changanya vijiko vitatu vya asali pamoja na kijiko kimoja cha mdalasini na pakaa kwenye chunusi.
Uwezo wa asali wa kuua bacteria utaufanya uso wako kuwa kawaida katika muda wa wiki mbili.



20.Kuumwa na wadudu {kwa washawasha} 

wenye sumu Pakaa asali na mdalasini moja kwa moja kwenye sehemu zilizoathirika na rudia wakati mwasho unapokuathiri. Rudia tena hadi viuvimbe vinatoweka.



21.Madhara ya ngozi {INFECTIONS}
Fanya kama ilivyoelekezwa hapo juu. Rudia kufanya hivyo hadi hali itakapokwisha.



22.Kupungua kwa uzito

Wawezakufurahia vyakula vyote unavyopenda, kuwa na afya nzuri na kupunguza uzito wa mwili ambao hauhitajiki kwa kula chakula chenye nguvu na ladha nzuri, kilichojaa vitu viwili muhimu vya asili ambavyo ni asali na mdalasini.unachohitajika kufanya ni kuhakikisha unavitumia vyote kwa kiasi katika mapishi yako. Vilevile, wataalamu wanasema unaweza kuondoa mabonge ya uvimbe wa nyamanyama nje ya mwili kwa kuanza siku yako kwa kutumia vijiko viwili vya asali iliyochanganywa na kijiko kimoja cha mdalasini ndani ya bilauri ya maji vuguvugu. Rudia mchanganyiko huu kabla ya kulala.

Wakati wa kipindi cha baridi kinapokaribia, ambacho kinaambatana na mazoezi machache, kuongeza hivi vitu viwili vya asili katika chakula ni muafaka. Pia kinywaji hiki vuguvugu kimeshahakikishwa na wataalamu wa lishe kwamba hupunguza hamu ya kula pamoja na kuleta joto mwilini.

23.Saratani {CANCER}

Utafiti uliomalizika karibuni huko Australia na Japan, umeonyesha kuwa asali ina uwezo mkubwa katika tiba ya mgonjwa anayetumia madawa ya kutibu saratani.

Katika tafiti iliyofanywa kwa wagonjwa waliokuwa wanaugua kwa kiwango kikubwa saratani ya mifupa na tumbo, wale waliokuwa wakitumia kila siku dozi za asali na mdalasini, walionyesha maradufu kupata nafuu kuliko wale waliokuwa wakitumia wakitumia madawa ya sarakani pekee. "Tuliwapa kijiko cha mdalasini na asali kutwa mara tatu kwa mwezi".anasema Dr Hiroki Owatta. "Wengine waliendelea na milo ya kawaida".




24.Uchovu {FATIGUE}
Upo ushahidi mpya kwamba sukari asilia zilizopo kwenye asali zina uwezo wa kuongeza nishati mwilini. Zikitumika ipasavyo, sukari hizi zinaweza kuwasaidia wazee na wengine wanaosumbuliwa na uchovu, wataalamu wanapendekeza kuchauganya nusu kijiko cha asali katika nusu bilauri ya maji, nyunyizia mdalasini na kunywa masaa mawili baada ya kuamka asubuhi. "Kunywa tena saa 9 alasiri wakati nishati {nguvu}inapoanza kushuka" anashauri Dr Milton Abbozza ambaye kazi zake kuhusu asali na mdalasini kama kichocheo cha nishati mwilini zinatambulika kimataifa. "katika wiki moja hii itajionyesha".



25.Kuvimba Nyayo {SORE FEET}

Chua asali na mdalasini vuguvugu katika {miguu} nyayo zilizoathirika baada ya siku ndefu na kazi au baada ya mazoezi marefu. Rudia kila asubuhi halafu nawisha nyayo kwenye maji baridi na vaa viatu.



26.Harufu mbaya kutoka mdomoni

Waamerica wa kusini wanasukutua kwa kutumia asali na mdalasini pamoja na vuguvugu kila asubuhi ili kufanya harufu toka mdomoni kuwa nzuri na safi kiasilia. Katika Asia ya kusini mashariki, watu hula kijiko cha mdalasini na asali ili kuondoa harufu mbaya mdomoni {halitosis}. Wataalamu wanaamini kwamba uwezo wa kuua bacteria uliopo kwenye asali ndiyo unaopigana na harufu mbaya itokayo mdomoni.


27.Kupungua kwa usikivu {HEARING LOSS}

Dozi za kila siku za asali na mdalasini hufanya hali ya usikivu kuwa makini kama ilivyogunduliwa na Wagiriki wa zamani.