Hakika ghadhabu hutokana (asili ya ) ya shetani, na hakika shetani kaumbwa kutokana na moto, na hakika moto unazimwa kwa maji, basi akighadhibika mmoja wenu na akatawadhe au anywe maji na ikiwezekana anyamanze kisha amlani shetani na kama hawezi kukaa katika sehemu hiyo basi aondoke penye mzozo huo ulio msababishia hiyo ghadhabu.
Mtume s.a.w atakae zuwia ghadhabu na yeye anaweza kuizuia basi ataitwa na mwenyezi mungu mtukufu juu ya vichwa vya viumbe siku ya kiama ( ewe fulani ), achagua katika mahurul-aini ( wanawake wa peponi ) ampendae.
Kwahiyo ndugu zangu tujifunze kuzuia hasira zetu ili tueze kufanikiwa siku ya qiyama, AAMIN.
FAIDA YA ASALI
Asali inafahamika vema Duniani kote kama mojawapo ya silaha ya kiajabu katika kupigana na magonjwa na matatizo yatokanayo na uzee. Sasa hivi, utafiti mpya umeonyesha kwamba uwezo wa asali unaweza kuongezwa maradufu kama itachanganywa na mdalasini wa kawaida.
Uchunguzi wa kina ufanywao kwa wiki na jarida la World News wa Tiba, wataalamu wa madawa yatokanayo na mimea pamoja na kijarida cha afya na lishe, imeonekana kwamba kuna dazani nyingi za umuhimu wa asali na mdalasini pamoja na michanganyiko {dawa} ya kusisimua iletayo afya bora.
Kama ifuatayo:
1. Ugonjwa wa Viungo/Maumivu na Uvimbe {ARTHRITIS}.
Wataalamu wa lishe wanapendekeza kuchukua kwa kutumia mchanganyiko wa sehemu moja ya asali pamoja na sehemu mbli za maji vuguvugu na kijiko kimoja {cha chai} chenye mdalasini - na kuchua sehemu zilizoathirika. Nafuu hupatikana katika muda wa dakika moja.
Vinginevyo tengeneza chai-kikombe kimoja chenye maji moto, weka vijiko vya chakula -viwili vya asali kwa kijiko cha chai cha mdalasini. Kunywa asubuhi na jioni ili kuondoa maumivu.
Katika tafiti iliyofanyika hivi karibuni na chuo kikuu kimoja huko Copenhagen, madaktari waliwapa wagonjwa 200, {syrup} mchanganyiko wa kijiko kimoja *cha chai* cha asali na kimoja cha mdalasini kila asubuhi kabla ya kifungua kinywa. Asilimia 73% yao waliripoti nafuu kubwa ya maumivu yao na ongezeko katika kufanya shughuli kama kujongea na kutembea vyema.
2. kukatika kwa nywele {HAIR LOSS}
Asali ikishachanganywa na mdalasini pamoja na mafuta vuguvugu ya olive, hutoa kichocheo maridhawa cha kuotesha nywele kinachotumika katika dawa ya Dork. Mchanganyiko huo vuguvugu unapakwa kwa kusugua kichwani na kuachwa kwa dakika 15.
3. Ukungu wa miguuni {FUNGUS}
Changanya kijiko kikubwa cha mezani cha asali, vijiko viwili vya mdalasini {vya chai}. Pakaa sehemu zilizoathirika usiku kwa muda wa nusu saa, kisha safisha kwa sabuni na maji. Shida yako itakwisha kwenye kipindi cha wiki moja.
4. Maambukizo kwenye kihofu cha mkojo {BLADDER INFECTION}
Bilauri ya maji vuguvugu yaliyochanganywa na vijiko viwili {vya chai} vya mdalasini na kijiko kimoja {cha chai} cha asali huondoa bacteria kwenye kibofu. Unaweza ukatumia juisi ya cranberry badala ya maji ikiwa ambukizo la kibofu linakuwa sugu.
5. Maumivu ya jino {TOOTHACHE}.
Changanya sehemu tano za asali, na sehemu moja ya mdalasini na tumia kwa maumivu ya jino.
Dondoshea kwenye jino au meno yaliyoathirika hadi maumivu yatakapotoweka.
6. Vidonda vitokanavyo kwa mgonjwa kulala kwa muda mrefu {CANKER
SORES}.
Saladi ya kupaka vidonda iliyochanganywa na asali pamoja na mdalasini kwenye chai ya raspberry
nyekundu ni dawa nzuri ya kuondoa maumivu makali ya canker sores.
7. Helemu {CHOLESTERAL}
Kipimo cha helemu cha watu waliokuwa na afya nzuri {katika jaribio} kilishuka kwa wastani wa asilimia 10 katika muda pungufu ya masaa mawili baada ya kunywa bilauri moja {ounce 16} yenye vijiko viwili vikubwa vya mdalasini iliyochanganywa na chai ya moto. Kinywaji hiki kutwa mara tatu kilifanya kazi nzuri ya kushusha kiwango cha helemu mwilini.
Mafua yameshaeleweka ya kwamba hupotea/huondoka baada ya masaa machache baada ya waathirika kutumia kijiko kimoja {cha mezani} cha asali vuguvugu iliyochanganywa na robo kijiko{cha chai} cha mdalasini, mchanganyiko huu ni mahususi katika kusaidia kuondoa chafya na kuvimba koo.
9. Ugumba {INFERTILITY}
Asali inaaminika kuamsha nyege na wapenzi wa jinsia zote mbili wanashauriwa kunywa anglao vijiko viwili {vya mezani} kila siku kabla ya muda wa kulala {usiku}.
Asali imetambuliwa kwa kipindi kirefu kama dawa ifaayo kuondoa mchafuko wa tumbo pamoja na kichefuchefu. Ongeza kiasi kidogo cha mdalasini na hii tiba ya kimaajabu vilevile itapunguza maumivu yaletwayo na vidonda vya tumbo.ll.Esidi/Gesi-Co2. Hco3. Hcl.
Kula asali pamoja na mdalasini huweza kuondoa mchafuko wa tumbo na utumbo uletwao na gesi kwa mujibu wa uchunguzi mahsusi iliofanywa huko India na Japan.
12.Ugonjwa wa Moyo {HEART DISEASE}
Unaweza kukinga kupata ugonjwa wa moyo na kuzuia mkusanyiko wa mtandao wa mafuta kwenye mishipa ya damu kwa kula asali na mdalasini mara kwa mara-kwa kupakaa wakati wa kifiingua kinywa.
Kula asali ya mkate wa ngano yenye nyuzinyuzi nyingi iliyopakwa kijiko kimoja {cha mezani} cha
mchanganyiko huo hapo juu kila siku. Tiba hii ya maajabu iliweza kupunguza kuganda kwa mishipa ya damu kwa 74% ya wagonjwa waliokuwa katika nyumba za kutunzia wagonjwa - utafiti mmoja ulionyesha.
Shinikizo la damu pamoja na matatizo yaambatanayo ya maumivu ya kifua na kizunguzungu yalitoweka kutoka kwa wagonjwa wengi wiki chache tu baada ya watafiti wa kitaliano kuwapa dozi za mara kwa mara za asali ilyochanganywa na mdalasini. Vipimo vya shinikizo la damu vilionyesha
ukawaida na wote 137 waliofanyiwa jaribio hilo waliripoti kujisikia vyema/vizuri baada ya wiki chache za tiba hii ya ajabu.
14.Kinga ya mwili {IMMUNE SYSTEM}
Kinga yako ya mwili itaongezeka mara tatu zaidi ikiwa utatumia mara kwa mara asali na mdalasini kwa pamoja - wataalamu wanasema.
Utafiti wa kitiba unaonyesha kwamba hazina kubwa ya vitamini{vivurutubisho} na madini pamoja na michanganyiko mingine iondoayo magonjwa pamoja na kinga itolewayo na chembechembe nyeupe za damu, husaidia kuzuia magonjwa pamoja na kuharibu vimelea {virus} na {bacteria}.
15.Ukosefu wa nguvu za kiume [Uhanithi]{IMPOTENCE}
Asali ina historia ndefu ya kuamsha uume pamoja na kuwa dawa madhubuti ya kuponyesha uhanithi.
Kutokana na uwezo wake kama kiamshaji/chaji, asali ilipigwa marufuku kwa makasisi katika baadhi ya dini za kimashariki mwa Dunia. Mwaka jana, watafiti wa kiaustralia waligundua kwamba asali ina uwezo wa kupeleka mwili kutoa homoni mbalimbali kama ilivyo kwa mdalasini, katika Africa na dunia ya kusini, mabaharia wamekuwa wakipaka asali katika sehemu zao za nje ya uume ili kuongeza stamina zao za kufanya mapenzi.
16.Kutokuchaguliwa kwa chakula {INDIGESTION}
Vijiko viwili vya asali iliyonyunyiziwa mdalasini kabla ya mlo{kula chakula} huondoa kiungulia na wataalamu wanasema kwamba asali husaidia kutolewa kwa juisi zinazotumika kuchaguliwa kwa vyakula tumboni na mdalasini unaongeza spidi ya kuchaguliwa kwa vyakula.
17.Flu {INFLTJENZA}
Tafiti moja ya kihispania imethibitisha kwamba aina ya dawa moja asilia ya ajabu ambayo huharibu vairasi {vimelea} waletayo Flu.
Unaweza kuishi kufikia hadi miaka 100 na kufurahia maisha ya afya na madhubuti kwa kunywa kila siku kikombe baridi cha chai ya mdalasini na asali. Kutengeneza kinywaji hiki kitamu, weka vijiko vine{vikubwa} vya mdalasini katika vikombe vitatu vya maji na koroga kwa dakika 10. kunywa robo kikombe kutwa mara tatu au nne na hivyo utakuwa na kinywaji kingi.
19.Chunusi {PIMPLES}
Changanya vijiko vitatu vya asali pamoja na kijiko kimoja cha mdalasini na pakaa kwenye chunusi.
Uwezo wa asali wa kuua bacteria utaufanya uso wako kuwa kawaida katika muda wa wiki mbili.
20.Kuumwa na wadudu {kwa washawasha}
wenye sumu Pakaa asali na mdalasini moja kwa moja kwenye sehemu zilizoathirika na rudia wakati mwasho unapokuathiri. Rudia tena hadi viuvimbe vinatoweka.
21.Madhara ya ngozi {INFECTIONS}
Fanya kama ilivyoelekezwa hapo juu. Rudia kufanya hivyo hadi hali itakapokwisha.
Wawezakufurahia vyakula vyote unavyopenda, kuwa na afya nzuri na kupunguza uzito wa mwili ambao hauhitajiki kwa kula chakula chenye nguvu na ladha nzuri, kilichojaa vitu viwili muhimu vya asili ambavyo ni asali na mdalasini.unachohitajika kufanya ni kuhakikisha unavitumia vyote kwa kiasi katika mapishi yako. Vilevile, wataalamu wanasema unaweza kuondoa mabonge ya uvimbe wa nyamanyama nje ya mwili kwa kuanza siku yako kwa kutumia vijiko viwili vya asali iliyochanganywa na kijiko kimoja cha mdalasini ndani ya bilauri ya maji vuguvugu. Rudia mchanganyiko huu kabla ya kulala.
Wakati wa kipindi cha baridi kinapokaribia, ambacho kinaambatana na mazoezi machache, kuongeza hivi vitu viwili vya asili katika chakula ni muafaka. Pia kinywaji hiki vuguvugu kimeshahakikishwa na wataalamu wa lishe kwamba hupunguza hamu ya kula pamoja na kuleta joto mwilini.
23.Saratani {CANCER}
Utafiti uliomalizika karibuni huko Australia na Japan, umeonyesha kuwa asali ina uwezo mkubwa katika tiba ya mgonjwa anayetumia madawa ya kutibu saratani.
Katika tafiti iliyofanywa kwa wagonjwa waliokuwa wanaugua kwa kiwango kikubwa saratani ya mifupa na tumbo, wale waliokuwa wakitumia kila siku dozi za asali na mdalasini, walionyesha maradufu kupata nafuu kuliko wale waliokuwa wakitumia wakitumia madawa ya sarakani pekee. "Tuliwapa kijiko cha mdalasini na asali kutwa mara tatu kwa mwezi".anasema Dr Hiroki Owatta. "Wengine waliendelea na milo ya kawaida".
24.Uchovu {FATIGUE}
Upo ushahidi mpya kwamba sukari asilia zilizopo kwenye asali zina uwezo wa kuongeza nishati mwilini. Zikitumika ipasavyo, sukari hizi zinaweza kuwasaidia wazee na wengine wanaosumbuliwa na uchovu, wataalamu wanapendekeza kuchauganya nusu kijiko cha asali katika nusu bilauri ya maji, nyunyizia mdalasini na kunywa masaa mawili baada ya kuamka asubuhi. "Kunywa tena saa 9 alasiri wakati nishati {nguvu}inapoanza kushuka" anashauri Dr Milton Abbozza ambaye kazi zake kuhusu asali na mdalasini kama kichocheo cha nishati mwilini zinatambulika kimataifa. "katika wiki moja hii itajionyesha".
Chua asali na mdalasini vuguvugu katika {miguu} nyayo zilizoathirika baada ya siku ndefu na kazi au baada ya mazoezi marefu. Rudia kila asubuhi halafu nawisha nyayo kwenye maji baridi na vaa viatu.
26.Harufu mbaya kutoka mdomoni
Waamerica wa kusini wanasukutua kwa kutumia asali na mdalasini pamoja na vuguvugu kila asubuhi ili kufanya harufu toka mdomoni kuwa nzuri na safi kiasilia. Katika Asia ya kusini mashariki, watu hula kijiko cha mdalasini na asali ili kuondoa harufu mbaya mdomoni {halitosis}. Wataalamu wanaamini kwamba uwezo wa kuua bacteria uliopo kwenye asali ndiyo unaopigana na harufu mbaya itokayo mdomoni.
27.Kupungua kwa usikivu {HEARING LOSS}
Dozi za kila siku za asali na mdalasini hufanya hali ya usikivu kuwa makini kama ilivyogunduliwa na Wagiriki wa zamani.
DAWA ZINAZO TIBU CHUNUSI
Dawa za Asili 10 zinazotibu chunusi
Chunusi
Chunusi ni ugonjwa wa ngozi ambao hujitokeza kama viuvimbe au vipele vidogo vidogo hasa sehemu za uso, kifuani na hata mgongoni.
Vipele hivi hutokea wakati vishimo vya kupitisha jasho katika ngozi vinapozibwa kwa mafuta au seli za ngozi zilizokufa au wadudu yaani bakteria.
Kwa lugha ya kidaktari chunusi huitwa Acne Vulgaris. Chunusi ndio ugonjwa wa ngozi ambao humwathiri binadamu kwa kiasi kikubwa kwa mfano nchini Marekani pekee huathiri watu zaidi ya milioni 17.
Chunusi huweza kujitokeza katika umri wowote lakini huathiri sana vijana hasa wakati wa balehe (adolescents).
1. Magadi Soda:
Magadi soda ni mazuri sana kwa kusafishia uso na haswa ukiwa na chunusi. Changanya kiasi kidogo cha magadi soda na maji ya kutosha kuunda kidonge kidogo na kisha weka au kandika kidonge hicho sehemu iliyoathirika na chunusi.
Kwa muda wa dakika 15 hadi 20 au mpaka ikauke, na kisha suuza kwa maji yasiyo ya moto. Unaweza kurudia rudia mara kadhaa kwa siku mpaka utakapoona athari za chunusi zimepotea.
2. Matango:
Unaweza kutumia Tango kwa kuondoa chunusi na hata kuondoa mabaka mabaka katika ngozi na kuifanya ngozi yako kuonekana yenye afya na yenye kuvutia.
Matango ni mazuri sana kwa kusafishia uso na haswa ukiwa na chunusi. Kata tango na kisha liponde ponde (unaweza kutumia blenda) kisha paka au kandika usoni. Acha likae kwa muda wa dakika 15 hadi 20 hivi, kisha suuza kwa maji baridi. Unaweza kurudia kwa siku mara mbili mpaka mara tatu hadi utakapopona.
3. Kitunguu Swaumu:
Unaweza kutumia kitunguu swaumu kuondoa chunusi. Matumizi ya Kitunguu swaumu huleta matokeo mazuri sana katika kuondoa chunusi usoni na hata kuuwa bakteria sababu kina kemikali (antiseptiki) inayozuia kukua kwa bakteria kwenye jeraha au ngozi iliyo athirika kwa chunusi au hata kwenye kidonda. Na pia ina viwango vya juu wa salfa (ni zuri kwa ajili ya kukausha mafuta kwenye ngozi ya mwili).
Twanga kitungu swaumu, au unaweza kukata nusu na kubandika sehemu iliyo na chunusi huku ukishikilia kwa dakika 5 mpaka 10, na kisha safisha na maji baridi. Waweza kufanya hivyo asubuhi na jioni.
4. Mnanaa (Peppermint):
Unaweza kutumia majani ya Mnanaa kuondoa chunusi usoni. Majani ya mnanaa hutumika hata kwa wale wenye matatizo ya Mba kwenye kichwa.
Twanga majani machache au saga kisha weka sehemu iliyo athirika. Wacha mpaka pakauke na kisha safisha kwa maji baridi. Unaweza kufanya hivyo mara kadhaa kwa siku.
5. Limao:
Kata limao na kisha kwa kutumia kijiti chenye pamba kiloweke kwenye maji ya limao, sugua sehemu yenye chunusi, kisha acha pakauke, unaweza kurudia rudia kila baada ya masaa kadhaa.
Usitumie maji ya limao ya kwenye chupa (ya dukani), kwa sababu yanaweza kuwa yamewekwa kemikali zingine ili kuyahifadhi kiasi cha kuondoa ubora wa kemikali halisi za kwenye limao. Tumia limao halisi.
6. Asali:
Matumizi ya asali kutibu chunusi huwezesha ngozi, iwe na afya na nyororo. Kwa sababu kwenye asali kuna virutubisho vingi vyenye kazi ya kuua vimelea (bacteria) na kuzuia uchafu na kusinyaa kwa ngozi.
Weka asali kidogo sehemu ilio athirika na iache kwa muda mrefu kadri uwezavyo. Vilevile unaweza kupaka uso mzima au hata mwili mzima ukitaka. Sababu asali inarutubisha ngozi ya mwili na kuifanya iwe na afya na mwonekano mzuri. Ukisha ridhika na muda wa asali kwenye ngozi yako unaweza kusafisha kwa kutumia maji ya vuguvugu.
7. Papai:
Unaweza kushangaa, lakini matumizi ya papai yameonyesha matokeo mazuri sana katika kuondoa chunusi usoni na kusafisha sehemu zingine za mwili.
Ponda ponda kiasi kidogo cha papai na upakae sehemu yenye chunusi, kisha liache kwa muda mrefu kadri uwezavyo. Ukisha ridhika na muda unaweza kujisafisha kwa kutumia maji ya kawaida. Unaweza kurudia mara kadhaa kila siku kama unataka.
8. Dawa Ya Meno:
Unaweza kushangaa, lakini ushangazwi na matokeo mazuri ya meno yako kusafishika kwa dawa ya meno.
Kemikali zinazotumika kuuwa Bakteria wa kwenye meno, pia zina uwezo wa kupambana na bakteria wengine. Tumia dawa ya meno isiyo na gel (non-gel) paka kwenye chunusi. Ni vizuri ukatumia usiku wakati wa kwenda kulala, ila si vibaya ukipaka hata muda wa asubuhi au mchana mradi tu uwe na muda wa kutosha wa dawa kukauka ili iweze kufanya kazi vizuri.
Namna nyingine ni kuchanganya dawa ya meno na unga wa mahindi au ngano iliyosagwa na kuwa laini sana. Unaweza kupaka na kuiacha ikauke kwa dakika tano mpaka 10.
Safisha kwa sabuni. Mchanganyiko huu unasaidia kukausha chunusi.
9. Poda:
Unaweza kutumia baby powder kwa kupaka nyakati za usiku wakati wa kwenda kulala na kuiacha mpaka asubuhi.
10. Mvuke:
Unaweza kutumia mvuke (Steam/vapour) kuondoa mafuta yaliozidi kwenye ngozi ya uso wako. Kwa kujifukisha. Kwa wale ambao hawana mashine wanaweza kujaza sufuria au bakuli kwa maji ya moto na kujifunika kwa taulo huku ukielekeza uso wako kwenye sufuria au bakuli lenye maji yanayotoa mvuke kwa dakika 5 mpaka 10 hivi. Unaweza kufanya hivi pamoja na njia mojawapo nilizo zitaja hapo juu.
MHIMU: Kunywa maji ya kunywa kila siku glasi 8 mpaka 10, jishughulishe na mazoezi ya viungo na ujiweke msafi kila mara.
Njia hizi za Asili zinaweza kuchukuwa muda kidogo mpaka kuona matokeo ya kuridhisha.
Njia zote hizi kama hazijaleta matokeo mazuri, tafadhali muone daktari wa ngozi au nenda hospitali iliyo karibu kwa uchunguzi zaidi wa ngozi yako.
Vipele hivi hutokea wakati vishimo vya kupitisha jasho katika ngozi vinapozibwa kwa mafuta au seli za ngozi zilizokufa au wadudu yaani bakteria.
Kwa lugha ya kidaktari chunusi huitwa Acne Vulgaris. Chunusi ndio ugonjwa wa ngozi ambao humwathiri binadamu kwa kiasi kikubwa kwa mfano nchini Marekani pekee huathiri watu zaidi ya milioni 17.
Chunusi huweza kujitokeza katika umri wowote lakini huathiri sana vijana hasa wakati wa balehe (adolescents).
1. Magadi Soda:
Magadi soda ni mazuri sana kwa kusafishia uso na haswa ukiwa na chunusi. Changanya kiasi kidogo cha magadi soda na maji ya kutosha kuunda kidonge kidogo na kisha weka au kandika kidonge hicho sehemu iliyoathirika na chunusi.
Kwa muda wa dakika 15 hadi 20 au mpaka ikauke, na kisha suuza kwa maji yasiyo ya moto. Unaweza kurudia rudia mara kadhaa kwa siku mpaka utakapoona athari za chunusi zimepotea.
2. Matango:
Unaweza kutumia Tango kwa kuondoa chunusi na hata kuondoa mabaka mabaka katika ngozi na kuifanya ngozi yako kuonekana yenye afya na yenye kuvutia.
Matango ni mazuri sana kwa kusafishia uso na haswa ukiwa na chunusi. Kata tango na kisha liponde ponde (unaweza kutumia blenda) kisha paka au kandika usoni. Acha likae kwa muda wa dakika 15 hadi 20 hivi, kisha suuza kwa maji baridi. Unaweza kurudia kwa siku mara mbili mpaka mara tatu hadi utakapopona.
3. Kitunguu Swaumu:
Unaweza kutumia kitunguu swaumu kuondoa chunusi. Matumizi ya Kitunguu swaumu huleta matokeo mazuri sana katika kuondoa chunusi usoni na hata kuuwa bakteria sababu kina kemikali (antiseptiki) inayozuia kukua kwa bakteria kwenye jeraha au ngozi iliyo athirika kwa chunusi au hata kwenye kidonda. Na pia ina viwango vya juu wa salfa (ni zuri kwa ajili ya kukausha mafuta kwenye ngozi ya mwili).
Twanga kitungu swaumu, au unaweza kukata nusu na kubandika sehemu iliyo na chunusi huku ukishikilia kwa dakika 5 mpaka 10, na kisha safisha na maji baridi. Waweza kufanya hivyo asubuhi na jioni.
4. Mnanaa (Peppermint):
Unaweza kutumia majani ya Mnanaa kuondoa chunusi usoni. Majani ya mnanaa hutumika hata kwa wale wenye matatizo ya Mba kwenye kichwa.
Twanga majani machache au saga kisha weka sehemu iliyo athirika. Wacha mpaka pakauke na kisha safisha kwa maji baridi. Unaweza kufanya hivyo mara kadhaa kwa siku.
5. Limao:
Kata limao na kisha kwa kutumia kijiti chenye pamba kiloweke kwenye maji ya limao, sugua sehemu yenye chunusi, kisha acha pakauke, unaweza kurudia rudia kila baada ya masaa kadhaa.
Usitumie maji ya limao ya kwenye chupa (ya dukani), kwa sababu yanaweza kuwa yamewekwa kemikali zingine ili kuyahifadhi kiasi cha kuondoa ubora wa kemikali halisi za kwenye limao. Tumia limao halisi.
6. Asali:
Matumizi ya asali kutibu chunusi huwezesha ngozi, iwe na afya na nyororo. Kwa sababu kwenye asali kuna virutubisho vingi vyenye kazi ya kuua vimelea (bacteria) na kuzuia uchafu na kusinyaa kwa ngozi.
Weka asali kidogo sehemu ilio athirika na iache kwa muda mrefu kadri uwezavyo. Vilevile unaweza kupaka uso mzima au hata mwili mzima ukitaka. Sababu asali inarutubisha ngozi ya mwili na kuifanya iwe na afya na mwonekano mzuri. Ukisha ridhika na muda wa asali kwenye ngozi yako unaweza kusafisha kwa kutumia maji ya vuguvugu.
7. Papai:
Unaweza kushangaa, lakini matumizi ya papai yameonyesha matokeo mazuri sana katika kuondoa chunusi usoni na kusafisha sehemu zingine za mwili.
Ponda ponda kiasi kidogo cha papai na upakae sehemu yenye chunusi, kisha liache kwa muda mrefu kadri uwezavyo. Ukisha ridhika na muda unaweza kujisafisha kwa kutumia maji ya kawaida. Unaweza kurudia mara kadhaa kila siku kama unataka.
8. Dawa Ya Meno:
Unaweza kushangaa, lakini ushangazwi na matokeo mazuri ya meno yako kusafishika kwa dawa ya meno.
Kemikali zinazotumika kuuwa Bakteria wa kwenye meno, pia zina uwezo wa kupambana na bakteria wengine. Tumia dawa ya meno isiyo na gel (non-gel) paka kwenye chunusi. Ni vizuri ukatumia usiku wakati wa kwenda kulala, ila si vibaya ukipaka hata muda wa asubuhi au mchana mradi tu uwe na muda wa kutosha wa dawa kukauka ili iweze kufanya kazi vizuri.
Namna nyingine ni kuchanganya dawa ya meno na unga wa mahindi au ngano iliyosagwa na kuwa laini sana. Unaweza kupaka na kuiacha ikauke kwa dakika tano mpaka 10.
Safisha kwa sabuni. Mchanganyiko huu unasaidia kukausha chunusi.
9. Poda:
Unaweza kutumia baby powder kwa kupaka nyakati za usiku wakati wa kwenda kulala na kuiacha mpaka asubuhi.
10. Mvuke:
Unaweza kutumia mvuke (Steam/vapour) kuondoa mafuta yaliozidi kwenye ngozi ya uso wako. Kwa kujifukisha. Kwa wale ambao hawana mashine wanaweza kujaza sufuria au bakuli kwa maji ya moto na kujifunika kwa taulo huku ukielekeza uso wako kwenye sufuria au bakuli lenye maji yanayotoa mvuke kwa dakika 5 mpaka 10 hivi. Unaweza kufanya hivi pamoja na njia mojawapo nilizo zitaja hapo juu.
MHIMU: Kunywa maji ya kunywa kila siku glasi 8 mpaka 10, jishughulishe na mazoezi ya viungo na ujiweke msafi kila mara.
Njia hizi za Asili zinaweza kuchukuwa muda kidogo mpaka kuona matokeo ya kuridhisha.
Njia zote hizi kama hazijaleta matokeo mazuri, tafadhali muone daktari wa ngozi au nenda hospitali iliyo karibu kwa uchunguzi zaidi wa ngozi yako.
HISTORIA YA UKHALIFA KATIKA UISLAMU.
Ndugu zangu katika masahaba wa mtume s.a.w wamegawanyika katika sehemu kuu mbili, ambazo ni answaar na muhajiriina, kwahiyo pindi alipo kufa mtume s.a.w wakaona answaari wazungumzie ukhalifa wa baada ya mtume.
Akasimama Saad ibn Ubada akazungumza na answar wenzake na kuwakumbusha fadhila za answar katika maisha ya mtume mpaka mtume s.a.w akasema" kama watu watafuata njia hii na answar wakafuata njia nyingine basi mimi mtume nitafuata njia ya answari", Saadi akazidi kuwakumbusha wenzie jinsi mtume alivyo kuwa anatupenda( answar ) kwahiyo tunahaki sisi ya kuwa viongozi baada ya mtume kuondoka.
Maongezi hayo yalikuwa yanafanyika katika jumba la banii saida,kwahiyo kipindi answar wakiendelea na mazungu mzo hayo baadhi ya muhajiriin hawakuwako katika eneo hilo la mazungumzo kama vile omar na abuu bakr, basi omar na abuu bakar walivyo pata taarifa kuwa kuna semina inayo endelea kufanyika katika jumba la banii saida wakawahi kwenda kusikiliza mazungumzo hayo, wakafika pale na kuona watu wanapanga kuhusu mambo ya uongozi baada ya mtume, lakini kipindi hicho hata mwili wa mtume ulikuwa haujazikwa.
Na hapa mayahudi walipata mdomo na kusema kuwambia waislamu kwamba " hakuna watu wabaya kama waislaamu, yaani hamjamzika mtume wenu mnaanza kugombania uongozi" walikuwa wakimwambia maneno hayo ally ibn abii twalib na ally ibn abii twalib akawajibu akawaambia " bora sisi waislamu tunagombea kumpata kiongozi atakae kuwa anatuongoza sisi katika mambo ya dini na dunia, ili hata katika mazishi ya mtume wetu tumsikilize yeye amiri wetu, kuliko ninyi mayahudi, pindi mungu alipo wapitisha katika bahari na akawaangamiza firauni na majeshi yake huku mnashuhudia lakini mlipo fika nchi kavu hata kabla maji hayaja kauka katika nyayo zenu, mnamwambia mussa, eewee mussa tutengenezee mungu wa sanamu kama walio kuwa wanaabudu babu zetu, huyo mnaetaka mtengenezewe ni nani na huyo alie waokoeni katika bahari ni nani? kwahiyo ally akawambia kati ya sisi na ninyi ni wapi wenye madhambi? mayahudi kwa jeuri yao hawakujibu swali hilo
Kwahiyo baada ya muda mfupi Abuu bakari akasimama katika semina hiyo na kuwapongeza answar kwa kile walicho kifanya na kuwaambia ni kweli mtume aliwapenda sana answar, hakuacha sifa abuu kakri ya answar siku hiyo ila zote alizitaja kisha akazitaja na sifa zote za muhaajiriin, lakini akawakumbusha kauli ya mtume alio bashiri kwamba" ni lazima kiongozi wenu atoke kwa makurayshi " na mtume alikuwa akilionyesha hilo mara mara, sasa mimi kama abuu bakri rai yangu ni kwamba amiri wetu atoke kwa makurayshi na mawaziri watoke kwa answar.
Baada ya rai hiyo ya abuu bakri, akasimama bwana mmoja anaitwa ubabu ibn mundhir akasema" haiwezezekani kisha ubabu akazidi kupaza sauti na kusema enyi watu wa answar ikiwa hao muhajiriin watapinga sisi kutupa uamiri na kutaka tuwe mawaziri basi lengo letu tunawaambia sisi (answar ) tuwe na amiri wetu na wao (muhajiriin) wawe na amiri wao.
Kisha baada ya hapo akasimama omary ibn khatwaab, akamwambia abuu ubabu kwamba watu wawili hawawezi kuongoza katika umma mmoja, kwahiyo bora apatikane mmoja alafu huyo mwingine awe waziri wake.
Kisha akasimama tena abuu ubabu ibn mundhir na kusema " enyi answar msiachilie kabisa suala hili, kama wamekataa suala la kuwa na sisi viongozi na wao viongozi basi nakwambieni answar kamateni hapo hapo,mkija mkakosea kidogo watakuja wachukue nafasi hii na heshima yenu ikakosekana.
kisha baada ya hapo akasimama bwana mmija anaitwa abuu ubeida ibn jarrah akasema," enyi watu wa answar nyie ndio watu wa mwanzo kumnusuru mtume, basi msiwe watu wa kwanza kusababisha fitna na chuki katika uislamu.
Kisha akasimama mmoja katika answar anaitwa bashiir ibn saad akasema, " enyi watu muhammad alikua ni mkureyshi katika kabila tukufu la maka na wale walio kuja nae kutoka makka, sisi tuka watukuza na kuwa kirimu mpaka tukapata heshima alio tupa mtume, basi na wao pia wanahaki ya kuwa nyuma ya mtume katika uongozi kuliko sisi, kama tumetangulia na kuzidi kuzidi kutangulia katika uislamu na tuka wanusuru ndugu zetu waislamu na tukapigana jihad mbali mbali katika uislamu, tumefanya hivyo kwa ajili ya kupata radhi za mwenyezi mungu, hatukufanya hivyo ili tuje tupate uongozi leo, kwanini magombania uamir?, kwanini tusisikilize viongozi ( muhajiriin ) wanavyo tuambia tukafuata ili tuzidi kupata kheri zaidi?
Alipo sema hayo wote wakanyamanza, pale pale akasimama abuu bakri na kukamata mkono wa omary na kuuinua juu, kisha akakamata mkono wa abuu ubeida na kuuinua juu akasema " mimi nimekuridhieni watu wawili hawa, chagueni mtu mmoja kati ya hawa awe amiri wetu.
omari akarudi nyuma na kusema " ewee abuu bakri mimi bora nipeleke kichwa changu kikatwe kuliko kuwa amiri mbele yako, wewe abuu bakri ndio unahaki ya kuwa khalifa kwasababu mtume alipo taka kutuongoza katika jambo lolote la dini alisema abuu bakri atuongoze awe imamu wetu, kama mtume karidhika abuu bakri atuongoze katika jambo la dini yetu kwanini sisi tusiridhike abuu bakri atuongoze katika jambo la dunia, wakati wa sala mtume amesema abuu bakri ndio asalishe, hi inaonesha mtume alitaka abuu bakri ndio awe kiongozi baada yake.
Omary alipotaka kuunyanyua mkono wa abuu bakri, yule answar ( bashiir ibn saad ) akawa yeye wa kwanza kuinua mkono wa abuu bakri kabla ya omary, kisha akafuata omary akainua mkono wa abuu bakri juu, kisha akafuata abuu ubeida kisha answar wote pamoja na muhajiriin wote walio kuwako pale wakasimama kwa ishara ya kwamba wameridhia abuu bakri kuwa kiongozi wao. yaani wote answar na muhajiriin wameridhia abuu bakri awe khalifa wao, neno amiril-muuminina halikuwako wakati huo kwasababu amiril-muuminiina limeanza wakati wa omary ibn khatwab, hapa alikuwa anajulikana kama khalifatu-rasuuli llah.
hapo ndipo uongozi rasmi wa abuu bakri ulipo anza na kuwa kalifa wa kwanza katika uislamu.
wallahu aalam.
Akasimama Saad ibn Ubada akazungumza na answar wenzake na kuwakumbusha fadhila za answar katika maisha ya mtume mpaka mtume s.a.w akasema" kama watu watafuata njia hii na answar wakafuata njia nyingine basi mimi mtume nitafuata njia ya answari", Saadi akazidi kuwakumbusha wenzie jinsi mtume alivyo kuwa anatupenda( answar ) kwahiyo tunahaki sisi ya kuwa viongozi baada ya mtume kuondoka.
Maongezi hayo yalikuwa yanafanyika katika jumba la banii saida,kwahiyo kipindi answar wakiendelea na mazungu mzo hayo baadhi ya muhajiriin hawakuwako katika eneo hilo la mazungumzo kama vile omar na abuu bakr, basi omar na abuu bakar walivyo pata taarifa kuwa kuna semina inayo endelea kufanyika katika jumba la banii saida wakawahi kwenda kusikiliza mazungumzo hayo, wakafika pale na kuona watu wanapanga kuhusu mambo ya uongozi baada ya mtume, lakini kipindi hicho hata mwili wa mtume ulikuwa haujazikwa.
Na hapa mayahudi walipata mdomo na kusema kuwambia waislamu kwamba " hakuna watu wabaya kama waislaamu, yaani hamjamzika mtume wenu mnaanza kugombania uongozi" walikuwa wakimwambia maneno hayo ally ibn abii twalib na ally ibn abii twalib akawajibu akawaambia " bora sisi waislamu tunagombea kumpata kiongozi atakae kuwa anatuongoza sisi katika mambo ya dini na dunia, ili hata katika mazishi ya mtume wetu tumsikilize yeye amiri wetu, kuliko ninyi mayahudi, pindi mungu alipo wapitisha katika bahari na akawaangamiza firauni na majeshi yake huku mnashuhudia lakini mlipo fika nchi kavu hata kabla maji hayaja kauka katika nyayo zenu, mnamwambia mussa, eewee mussa tutengenezee mungu wa sanamu kama walio kuwa wanaabudu babu zetu, huyo mnaetaka mtengenezewe ni nani na huyo alie waokoeni katika bahari ni nani? kwahiyo ally akawambia kati ya sisi na ninyi ni wapi wenye madhambi? mayahudi kwa jeuri yao hawakujibu swali hilo
Kwahiyo baada ya muda mfupi Abuu bakari akasimama katika semina hiyo na kuwapongeza answar kwa kile walicho kifanya na kuwaambia ni kweli mtume aliwapenda sana answar, hakuacha sifa abuu kakri ya answar siku hiyo ila zote alizitaja kisha akazitaja na sifa zote za muhaajiriin, lakini akawakumbusha kauli ya mtume alio bashiri kwamba" ni lazima kiongozi wenu atoke kwa makurayshi " na mtume alikuwa akilionyesha hilo mara mara, sasa mimi kama abuu bakri rai yangu ni kwamba amiri wetu atoke kwa makurayshi na mawaziri watoke kwa answar.
Baada ya rai hiyo ya abuu bakri, akasimama bwana mmoja anaitwa ubabu ibn mundhir akasema" haiwezezekani kisha ubabu akazidi kupaza sauti na kusema enyi watu wa answar ikiwa hao muhajiriin watapinga sisi kutupa uamiri na kutaka tuwe mawaziri basi lengo letu tunawaambia sisi (answar ) tuwe na amiri wetu na wao (muhajiriin) wawe na amiri wao.
Kisha baada ya hapo akasimama omary ibn khatwaab, akamwambia abuu ubabu kwamba watu wawili hawawezi kuongoza katika umma mmoja, kwahiyo bora apatikane mmoja alafu huyo mwingine awe waziri wake.
Kisha akasimama tena abuu ubabu ibn mundhir na kusema " enyi answar msiachilie kabisa suala hili, kama wamekataa suala la kuwa na sisi viongozi na wao viongozi basi nakwambieni answar kamateni hapo hapo,mkija mkakosea kidogo watakuja wachukue nafasi hii na heshima yenu ikakosekana.
kisha baada ya hapo akasimama bwana mmija anaitwa abuu ubeida ibn jarrah akasema," enyi watu wa answar nyie ndio watu wa mwanzo kumnusuru mtume, basi msiwe watu wa kwanza kusababisha fitna na chuki katika uislamu.
Kisha akasimama mmoja katika answar anaitwa bashiir ibn saad akasema, " enyi watu muhammad alikua ni mkureyshi katika kabila tukufu la maka na wale walio kuja nae kutoka makka, sisi tuka watukuza na kuwa kirimu mpaka tukapata heshima alio tupa mtume, basi na wao pia wanahaki ya kuwa nyuma ya mtume katika uongozi kuliko sisi, kama tumetangulia na kuzidi kuzidi kutangulia katika uislamu na tuka wanusuru ndugu zetu waislamu na tukapigana jihad mbali mbali katika uislamu, tumefanya hivyo kwa ajili ya kupata radhi za mwenyezi mungu, hatukufanya hivyo ili tuje tupate uongozi leo, kwanini magombania uamir?, kwanini tusisikilize viongozi ( muhajiriin ) wanavyo tuambia tukafuata ili tuzidi kupata kheri zaidi?
Alipo sema hayo wote wakanyamanza, pale pale akasimama abuu bakri na kukamata mkono wa omary na kuuinua juu, kisha akakamata mkono wa abuu ubeida na kuuinua juu akasema " mimi nimekuridhieni watu wawili hawa, chagueni mtu mmoja kati ya hawa awe amiri wetu.
omari akarudi nyuma na kusema " ewee abuu bakri mimi bora nipeleke kichwa changu kikatwe kuliko kuwa amiri mbele yako, wewe abuu bakri ndio unahaki ya kuwa khalifa kwasababu mtume alipo taka kutuongoza katika jambo lolote la dini alisema abuu bakri atuongoze awe imamu wetu, kama mtume karidhika abuu bakri atuongoze katika jambo la dini yetu kwanini sisi tusiridhike abuu bakri atuongoze katika jambo la dunia, wakati wa sala mtume amesema abuu bakri ndio asalishe, hi inaonesha mtume alitaka abuu bakri ndio awe kiongozi baada yake.
Omary alipotaka kuunyanyua mkono wa abuu bakri, yule answar ( bashiir ibn saad ) akawa yeye wa kwanza kuinua mkono wa abuu bakri kabla ya omary, kisha akafuata omary akainua mkono wa abuu bakri juu, kisha akafuata abuu ubeida kisha answar wote pamoja na muhajiriin wote walio kuwako pale wakasimama kwa ishara ya kwamba wameridhia abuu bakri kuwa kiongozi wao. yaani wote answar na muhajiriin wameridhia abuu bakri awe khalifa wao, neno amiril-muuminina halikuwako wakati huo kwasababu amiril-muuminiina limeanza wakati wa omary ibn khatwab, hapa alikuwa anajulikana kama khalifatu-rasuuli llah.
hapo ndipo uongozi rasmi wa abuu bakri ulipo anza na kuwa kalifa wa kwanza katika uislamu.
wallahu aalam.
Subscribe to:
Posts (Atom)